1. 1.
    +1
    (verse:1)

    Ee Mungu nguvu yetu
    Ilete baraka kwetu

    Haki iwe ngao na mlinzi
    Natukae na udugu

    Amani na uhuru
    Raha tupate na ustawi.

    (verse:2)

    Amkeni ndugu zetu
    Tufanye sote bidii

    Nasi tujitoe kwa nguvu
    Nchi yetu ya Kenya

    Tunayoipenda
    Tuwe tayari kuilinda

    (verse:3)

    Natujenge taifa letu
    Ee, ndio wajibu wetu

    Kenya istahili heshima
    Tuungane mikono

    Pamoja kazini
    Kila gibu tuwe na shukrani
    ···
   tümünü göster